NALA, Kampuni ya Mtanzania Benji Fernandes Yapata Uwekezaji wa Bilioni 100



Kampuni ya kutuma na kupokea fedha ya NALA iliyoanzishwa na Mtanzania Benji Fernandes imepata uwekezaji wa dola za kimarekani milioni 40 sawa na Sh. bilioni 100 hii ni baada ya kampuni hiyo kuendelea kufanya vyema katika kuwezesha mzunguko wa fedha Afrika.
Muendelezo huu wa mafanikio ya kampuni hii unakuja ikiwa ni miaka miwili tu toka kampuni hiyo iweze kupokea uwekezaji wa dola milioni 10 (Bilioni 23) mnamo Januari 2022.
Akielezea juu ya mafanikio hayo, Mkurugenzi wa Nala anasema, ‘kazi yao bado haijafikia mwisho’, huku akiorodhesha changamoto mbalimbali watu wanazokutana nazo wakitaka kutuma fedha Afrika, hasa uwepo wa makampuni mbalimbali na mabenki yasiyokuwa na mawasiliano ya pamoja.


