
Timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ imepoteza kwa magoli 2-0 licha ya kuwa nyumbani kwenye Uwanja wa Mkapa ikicheza dhidi ya Morocco katika mchezo wa Kundi E Kuwania Kufuzu Kombe la Dunia 2026.

Magoli yamefungwa na Hakim Ziyech anayeitumika Galatasaray ya Uturuki na Lusajo Mwaikenda wa Azam FC aliyejifunga.
Matokeo mengine ya Kundi E, Niger imeifunga Zambia magoli 2-1, hivyo timu zote hizo zina pointi tatu kasoro Congo ambayo haina alama.



