

BAO pekee la kiungo Mbrazil, Bruno Gomez dakika ya 45 limeipa Singida Big Stars ushindi wa 1-0 dhidi ya Azam FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara leo Uwanja wa LITI, Singida.
Kwa ushindi huo, Singida Big Stars inafikisha pointi 43, ingawa inabaki nafasi ya nne ikizidiwa tu wastani wa mabao na Azam FC baada ya wote kucheza mechi 21.



