▶️DONDOO ZA JIKONI:-
1 Ukiandaa nyama kwa viungo kama tangawizi, thomu na masala ongeza mafuta kidogo na mtindi vijiko viwili utafurahi.
2 Ukikosa vanilla unaweza saga ganda la limao bichi linaleta harufu nzuri kwenye keki na chapati za maji.
3 Ukipika mboga ya karanga tumia maziwa kukorogea karanga badala ya maji inanoga.
4 Ukiunguza wali penyeza mapande makubwa ya pilipili hoho inatoa kbs harufu ya kuungua.
5 Ukiona mafuta yamezidi kwenye supu au mchuzi tumia mkate wa silesi kupitisha kwa juu itanyonya mafuta.
6 Ukitaka maharage yawe na rojo zuri pale unapoyachemsha weka na mafuta ya kupikia kidogo yawive pamoja.
7 Ukitengeneza juice ya rosela au ubuyu chemshia pamoja na mchaichai inakuwa nzuri sana.
8 Chapati ikilala ukitaka kuipasha iwe laini ichovye kwenye maji baridi na uipashe bila mafuta itakuwa kama ndio umeipika muda huo.
9 Ukipika matembele jaribu kuweka tangawizi na pilipili manga utajionea maajabu.
10 Ukitaka samaki wabichi wasivurugike au kung’ang’ania kwenye chuma unapowakaanga tengeneza rojo ya ngano wachovye pia huwa ni watamu sana.
11 Ukitaka utumbo iwive haraka weka limao bila ya chumvi kwa yale maji ya kwanza.
12 Chumvi ikizidi kwenye mchuzi menya kiazi mbatata weka ganda lake acha uchemke chumvi itapungua sana.
13 Maharage ukitaka yawive upesi weka kijiko kimoja cha baking powder.
14 Mchuzi ukitaka uwe na rojo zito na huna nyanya za kutosha koroga kijiko kimoja cha unga wa ngano weka na acha uchemke.
15 Muhogo ukiwa chelema weka kijiko kimoja cha baking powder.
16 Nyama ikiwa ngumu au ukitaka ilainike vizuri kwangulia papai bichi.
17 Karoti zikisinyaa kwa kukaa muda mrefu ziweke kwenye maji baridi kwa nusu saa zitakuwa kama zimetoka shamba.
18 Kama unatumia jiko la gas kupikia basi tumia maji baridi kupikia wali utaona mambo.
19 Ukiunguza wali kwa mara nyingine kata kitunguu maji nusu kiweke katikati harufu ya kuungua hutoweka.



